Pages

UKATILI>> SUMBAWANGA,MANESI WAWAPIGA WAZAZI KWA KUWALAZIMISHA KUSUKUMA MTOTO.



Huu ni ukatili ambao wanafanyiwa wajawazito si kule Rukwa pekee, bali nchini kwa jumla
Sumbawanga. Siyo jambo geni kusikia wanawake wakiwalalamikia wauguzi ama kwa kuwapiga au kuwatukana wakati wa kujifungua.
Hata hivyo, matukio ya mama kupoteza maisha ama mtoto aliye tumboni kufariki kwa ajili ya vitendo hivyo vimekuwepo, lakini siyo kwa wingi.
Rehema Michael (18), mkazi wa Kijiji cha Tentula Sumbawanga Vijijini ni mmoja kati ya waliokutana na chungu ya kutukanwa na kupigwa na muuguzi wakati wa kujifungua.
Rehema ambaye ilikuwa ni mimba yake ya kwanza, amepoteza mtoto na yeye mwenyewe kunusurika kifo kutokana na hali yake.
Rehema akiwa mchovu anasimulia kwa uchungu kisa chote tangu alipopata uchungu wa kujifungua mpaka alipofikishwa hospitali.
“Nilisikia uchungu siku ya Jumatatu, nikamwambia mama mkwe ,tukaondoka naye kwenda kwenye zahanati ya pale kijijini Tentula.
“Tulipofika hatukumkuta muuguzi wa zamu na daktari tuliyemkuta hakuwa na funguo ya chumba kwa hiyo akatubeba kwenye pikipiki mpaka kwenye kituo cha afya cha Ikozi.
“Nilipofika hapo nikaingizwa kwenye chumba cha kuzalia, nikawa najitahidi kusukuma mtoto, nesi akanipiga ili nisukume mtoto, nilijitahidi kusukuma mtoto mpaka kichwa kikaanza kutoka  hadi kufikia kidevu, lakini kwa kuwa nilivyokuwa napigwa nikaishiwa nguvu.
Muuguzi akaniambia niache uvivu, “Sukuma, acha ujinga, nani alikutuma?” akaendelea hivyohivyo, kwa kweli nilikuwa nasikia maumivu sana.
Nilipoishiwa nguvu aliendelea kunipiga ili nisukume mtoto, lakini nikashindwa ndiyo ikabidi gari liitwe ili niletwe hapa kwenye hospitali ya mkoa.
Nilifika huko mtoto akining’inia, hivyo mpaka ninafika hapo, nilipotoka huko mpaka mtoto alikuwa hai, lakini mpaka nafikikishwa hapo, nikaambiwa mtoto ameshakufa.