Huru hatimaye
1990
Jamii ya kimataifa iliiwekea vikwazo zaidi serikali ya
ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini. Vikwazo vya kwanza viliwekwa
mwaka 1967.Shinikizo zilizaa matunda na mnamo mwaka 1990, rais FW De
Klerk akakiondolea marufuku chama cha ANC. Tarehe 11 Februari, Mandela
aliachiliwa baada ya miaka 27 jela. Umati wa watu ulimshangilia huku
yeye pamoja na mkewe wakiondoka sehemu ya jela. Katika mkutano wa kwanza
wa chama cha ANC mwaka uliofuata, Mandela alichaguliwa kama kiongozi wa
chama .Mazungumzo yakaanza ya kuunda serikali ya pamoja ya waafrika
weusi na wazungu.
4 kati ya 10
0 comments:
Post a Comment