MFALME wa mistari, Selemani Msindi ‘Afande Sele,’ amesema yuko
mbioni kuachia filamu yake mpya itakayofahamika kwa jina la ‘Filamu
Yangu.’
Akizungumza jana na Tanzania Daiama, Afande Sele alisema kuwa filamu hiyo itazungumzia maisha halisi ya Kitanzania.
Alisema ameamua kujikita katika uigizaji wa filamu kutokana na filamu
nyingi za sasa kutokuwa na maadili halisi ya Kitanzania, hivyo anataka
kuonyesha njia.
“Mimi nikiangalia filamu za hao wanaojiita ma-superstar, sifiki
mwisho na sijawahi kuangalia filamu yoyote ya kibongo hadi mwisho,
zinaboa na unaona hakuna uhalisia wa jambo husika, watu wanaiga
Wanigeria mwanzo-mwisho, wanakera,” alisema.
Afande Sele alisema kuwa ujio wa ‘Filamu Yangu’ utakuwa wa tofauti
kuanzia picha, maadili na namna wasanii wake watakavyoigiza...............
Aliwataka Watanzania kukaa mkao wa kula kwani filamu hiyo ipo jikoni ikipikwa kwa ustadi mkubwa.
0 comments:
Post a Comment