Pages

MTUMIKIE KAFIRI UPATE MRADI WAKO, JK,AOMBA SURUHU KWA YOWERI MUSEVEN.



RAIS Jakaya Kikwete amemuomba Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Rais Yoweri Museveni wa Uganda, kuwa msuluhishi wa mgogoro wa chini kwa chini unaoendelea kati ya Tanzania na Rwanda.(P.T)

Uamuzi huo, ulitangazwa bungeni mjini Dodoma jana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pinda alitangaza uamuzi huo, wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu ambapo Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alitaka kujua hatua za Serikali katika kile kinachoonekana Tanzania kutaka kutengwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mbowe, alisema hatua ya nchi za Rwanda, Kenya na Uganda kuendesha vikao kupitia wakuu wa nchi ikiwemo kujitoa kwa nchi ya Rwanda kutumia Bandari ya Dar es Salaam, kunaashiria mwelekeo mbaya

0 comments:

Post a Comment